Tuesday, April 25, 2017

NI NANI MSHTAKI WA ADUI YAKO?


Siku ya leo ningeomba tafakati yetu tukiongozwa na kitabu cha Esta wakati wa mfalme Ahausero ambapo Esta alichaguliwa kua malkia. “Mfaime akampenda Esta kuliko wanawake wote, naye akapata neema na kibali machoni pake kuliko mabikira wote; basi akamria taji ya kifaime kichwani pake, akamfanya awe malkia badala ya Vashti” (Esta 2:17). Katika kipindi hiki cha ufalme ndipo amri ilitoka kwa mkuu wa maakida aitwae Hamani bin Hamedatha kua wayahudi wote kuangamizwa (Esta 3:6) akiwemo Malkia Esta pasipo kujua ni myahudi.
Katika maisha yetu ya kila siku kabla ya kuumbwa kwetu Mwenyezi Mungu alitujua kabla “Kabla sijakuumba ndani ya tumbo la mama yako nalikujua, na kabala hujazaliwa , nilikutakasa, na kukuweka uwe nabii wa mataifa” (Yeremia 1:5) Hivyo basi anayajua wazi mambo yanayotunyong’onyesha, anayajua vyema ambayo yanatukatisha tamaa na kutueka mbali na yeye. “Hamani” apa huenda ikawa ni hali ya ndoa yako, huenda ikawa ni hali ya kipato chako cha kazi, au huenda ikawa ni uhusiano wako katika famila yako,rafiki jamaa na majirani, Hamani anaweza akawa ni matokeo yako shuleni au matokeo duni ya mipanago yako ya kimaisha, afya yako. Mambo ambayo yanatufanya tuwe mbali na Mwenyez Mungu kwa kutenda dhambi kupitia hayo, kwa namna ya kutegemea mawazo yetu binafsi na kumsahau yeye muweza wa yote.
Mungu anajua kupanda kwako na kushuka kwako, anaijua ilipo huzuni yako na anajua ilipo furaha yako na ndio maana akatupa zawadi pekee ya pendo lake na kwa hilo ashibisha roho zetu. Ametupatia kibali tangu kuumbwa kwetu kwa sura na mfano wake kisha kutufanya wafalme tutawale viumbe vyote, ndege wa angani, samaki wa baharini na wanyama wa porini (Mwanzo 1:26)
Esta kwa kibali alichopata mbele ya mfalme Ahausero aliweza mshtakia amani juu ya mtesi wake. Alimshtakia Hamani juu ya adhma yake ya kutaka kuwaangamiza wayahudi wote pamoja na yeye. aliweza kwa kuongoza na roho wa Mungu kwa sala na toba zilifanywa na wayahudi wote. (Esta 7:1-6)
Anatulika sote kusemezana nae, huu ni mualiko muhim kwetu hasa kwa njia ya imani thabiti iliojengeka mioyo yenu mwetu kwa njia ya kusikia neon lake. Anatualika tumshtaki ‘Hamani’ wetu ni yapi yanayotuangusha, yapi yanayotukatisha tamaa, yapi yanayotueka mbali na pendo lake, ni yapo yanataka kutuanagamiza hasa katika sala. Katika sala tunaweza kushukuru kwa mema mengi Mwenyez Mungu aliotujalia, pia katika sala tunaweza kumueleza masumbuko yetu.          Tuombe
“Nakushukuru Mungu kwa zawadi ya upendo wako kwengu, na kwa ajili ya mema mengi ulionijalia. Mbele zako naziweka shida/masumbuko yangu …(zitaje) nikiamin kua wewe ni mwanzo na mwisho, muweeza wa yote. Nikiomba nguvu mpya na hekima nizidi kupata neema zako nikitegemea msaada wako nikiyashinda yote kadiri ya mapenzi yako. Nikiomba hayo yote kwa njia ya Kristu bwana wetu……….”Amina

Novath Ngowi

No comments:

Post a Comment

Sefania 3:17 "Yehova Mungu wako yupo katikati yako. Kama Mwenye nguvu, ataokoa.Atakufurahia kwa shangwe. Atanyamaza katika upendo wake...