Sunday, April 9, 2017

Karibu Blogu ya Tumaini Jipya


Karibu katika ukurasa huu wa blogu uitwao TUMAIN JIPYA. Awali ya yote ningependa kumshukuru mwenyezi  Mungu  kwa wingi wa neema na rehema na kwa zawadi kubwa ya uhai aliotujalia mimi na wewe na watu wake wote kwa ujumla. Katika safari ya maisha hapa duniani alitupatia zawadi hii ya uhai ili tuweze kumjua  yeye , tumpende, tumtumikie yeye tukiwa hapa na siku ya mwisho baada ya yote turudi kwake  (Yn 14:3). Tumepata nafasi kubwa kuwa viumbe wa kipekee, tulioumbwa kwa sura na mfano wa mwenyezi Mungu, kisha akatufanya wafalme wenye kutawala vyote samakiwa baharini, ndege wa angani na wanyama na vyote (Mwanzo 1:26). Kwa namna hiyo tumekabidhiwa wajibu wa kutumikiana sisi kwa sisi, tukikumbushana kazi ya wokovu, kupendana, kushirikishana kwa kutiana moyo katika kila changamoto za kimaisha katika safari yetu ya hapa duniani, tukijua ya kwamba ipo tuzo kwa kupigana vita vilivyo vizuri. (2Timotheo 4:8)
Zipo changamoto nyingi za kimaisha tunazopitia kila siku, kubwa na ndogo, zote hizi zipo kwa namna ya kutujenga kwa akututia nguvu na kutukumbusha kua yupo Baba aliesimama nasi na kupigana kwa ajili yetu sisi tukiwa na jukumu la kuilinda Imani, “Lakin mwenye kuvumilia hata mwisho, ndie atakaeokoka’’ (Mt 24:13)
Ningependa kukwambia kua lipo TUMAINI JIPYA, ipo amani katika familia yako, lipo tumaini katika kazi yako, upo ushindi  katika masomo yako, upo upendo katika ndoa yako, upo ushindi katika ndoto zako. Kama ilivyoandikwa kwenye kitabu cha nabii Isaya 41:10 “Usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam nitakushika kwa mkonowa kuume wa haki yangu”. Tusifadhaike mioyoni mwetu, kwa Yesu Kristu ipo faraja, lipo pumziko na ushindi.
Ningependa kukukaribisha tena, tukishirikishana upendo wa Kristu na kuonja raha ya TUMAINI JIPYA chini ya njia ya msalaba kwa masomo na tafakari za biblia.
  
       Karibu!

No comments:

Post a Comment

Sefania 3:17 "Yehova Mungu wako yupo katikati yako. Kama Mwenye nguvu, ataokoa.Atakufurahia kwa shangwe. Atanyamaza katika upendo wake...