Karibu katika ukurasa huu
wa blogu uitwao TUMAIN JIPYA. Awali ya
yote ningependa kumshukuru mwenyezi Mungu
kwa wingi wa neema na rehema na kwa
zawadi kubwa ya uhai aliotujalia mimi na wewe na watu wake wote kwa ujumla. Katika
safari ya maisha hapa duniani alitupatia zawadi hii ya uhai ili tuweze kumjua yeye , tumpende, tumtumikie yeye tukiwa hapa
na siku ya mwisho baada ya yote turudi kwake (Yn 14:3). Tumepata nafasi kubwa kuwa viumbe
wa kipekee, tulioumbwa kwa sura na mfano wa mwenyezi Mungu, kisha akatufanya wafalme
wenye kutawala vyote samakiwa baharini, ndege wa angani na wanyama na vyote
(Mwanzo 1:26). Kwa namna hiyo tumekabidhiwa wajibu wa kutumikiana sisi kwa
sisi, tukikumbushana kazi ya wokovu, kupendana, kushirikishana kwa kutiana moyo
katika kila changamoto za kimaisha katika safari yetu ya hapa duniani, tukijua
ya kwamba ipo tuzo kwa kupigana vita vilivyo vizuri. (2Timotheo 4:8)
Zipo changamoto nyingi za
kimaisha tunazopitia kila siku, kubwa na ndogo, zote hizi zipo kwa namna ya
kutujenga kwa akututia nguvu na kutukumbusha kua yupo Baba aliesimama nasi na
kupigana kwa ajili yetu sisi tukiwa na jukumu la kuilinda Imani, “Lakin mwenye
kuvumilia hata mwisho, ndie atakaeokoka’’ (Mt 24:13)
Ningependa kukwambia kua
lipo TUMAINI JIPYA, ipo amani katika
familia yako, lipo tumaini katika kazi yako, upo ushindi katika masomo yako, upo upendo katika ndoa
yako, upo ushindi katika ndoto zako. Kama ilivyoandikwa kwenye kitabu cha nabii
Isaya 41:10 “Usiogope, kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike, kwa maana
mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia, naam nitakushika kwa
mkonowa kuume wa haki yangu”. Tusifadhaike mioyoni mwetu, kwa Yesu Kristu ipo
faraja, lipo pumziko na ushindi.
Ningependa kukukaribisha
tena, tukishirikishana upendo wa Kristu na kuonja raha ya TUMAINI JIPYA chini
ya njia ya msalaba kwa masomo na tafakari za biblia.
Karibu!
No comments:
Post a Comment